Thursday, December 7, 2017

Waziri Jafo: Wanafunzi 650,862 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza 2018



Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - TAMISEMI Selemani Jafo amesema kuwa jumla ya wanafunzi 650,862 waliofaulu mtihani wa darasa la saba uliofanyika mwezi Septemba 2017 wamefanikiwa kuchaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza katika awamu ya kwanza mwaka wa masomo 2018.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma, Waziri Jafo amesema wanafunzi  hao waliochaguliwa kwa awamu ya kwanza ni sawa na asilimia 98.31 kati ya wanafunzi waliofaulu mtihani huo na kuwataja wanafunzi wengine 11,173  sawa na asilimia 1.69 ya waliofaulu hawakuweza kupata nafasi ya kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika awamu hiyo kutokana na uhaba wa miundombinu.

Amesema idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu imeongezeka kwa jumla ya wanafunzi 124,209 likiwa ongezeko la asilimia 23.58 ikilinganishwa na wanafunzi 526,653 waliochaguliwa awamu ya kwanza mwaka huu.

Aidha, amesema baadhi ya wanafunzi wa mikoa ya Lindi, Mbeya, Rukwa, Manyara, Katavi na Simiyu, wamekosa nafasi kutokana na uhaba wa miundombinu ya elimu katika mikoa yao vikiwemo vyumba vya madarasa.

No comments:
Write comments

Matangazo

Matangazo
Loading...