Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo, Mhe. Samia amewaasa vijana kuacha kujihusisha na ngono zembe ili kuepuka kuendelea kuambukizwa ukimwi na kudhibiti maambukizi mapya ya ugonjwa huo hatari duniani kote.
Aidha, Makamu wa Rais amewataka akina dada wanaofanya biashara za kuuza miili yao kingono (machangudoa) kuacha mara moja kwani kufanya hivyo kutapelekea kupoteza nguvu kazi la kesho.
Kitaifa Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yamefanyika leo katika Mkoa wa Lindi ambapo Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewaongoza Watanzania wote katika katika maadhimisho hayo..
No comments:
Write comments