Tuesday, August 29, 2017

TFF watoa Ngao mpya kwa Simba


Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limefanya marekebisho katika Ngao ya Jamii ambayo timu ya Simba ilikabidhiwa baada ya kuifunga Yanga siku ya  Jumatano ya wiki iliyopita.

Awali Ngao hiyo ilikosewa katika kuandika neno SHIELD na kuandikwa SHELD Simba walikabidhiwa lakini baada ya makosa kuonekana TFF waliomba radhi siku iliyofuata kisha kuwaambia Simba wairejeshe Ngao hiyo kwa ajili ya marekebisho ya neno hilo.

Ofisa Habari wa TFF  Alfred Lucas ameionyesha Ngao iliyorekebishwa kwa waandishi wa habari leo Jumanne kwenye ofisi za shirikisho hilo Karume jijini Dar.

No comments:
Write comments

Matangazo

Matangazo
Loading...